KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 25, 2015

HATA KAMA MKE WA MTU NI SUMU, KIFO CHA MWENYEKITI WA ACT HUKO KATAVI NI CHA KINYAMA SANA


Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari
Kamanda Kidavashari

MWENYEKITI wa kitongoji cha Songambele katika wilaya ya Mlele mkoani Katavi kupitia chama cha ACT, Richald Madirisha (31) ameuawa kwa kuchinjwa na kiwiliwili chake kutenganishwa akituhumiwa kunyang’anya mke wa mtu.
Baada ya mauaji hayo, viungo vyake vya mwili vikiwamo mikono, kichwa, miguu na sehemu zake za siri vilichemshwa kwenye sufuria mithili ya nyama inavyopikwa nje ya nyumba yake.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari, amethibitisha kutokea kwa mkasa huo na kuongeza kuwa mauaji hayo yalifanyika juzi saa tano na nusu usiku nyumbani kwa marehemu katika kitongoji hicho cha Songambele.
Kamanda Kidavashari alisema hayo jana alipozungumza na mwandishi wa habari hizi kwa simu mjini Mpanda mkoani Katavi. “Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha mauaji kimetokana na visa vya marehemu na mtu mmoja, ambaye walikuwa wakiishi pamoja ambaye alikuwa akimtuhumu marehemu kuwa amemnyang’anya mwanamke ambaye alikuwa na uhusiano naye kimapenzi.
“Madirisha aliamua kuhama naye kijijini hapo na kuhamia naye kijiji cha Songambele katika wilaya Mlele,” alisema Kamanda Kidavashari.
Kwa mujibu wa Kamanda Kidavashari, siku ya tukio Madirisha alikuwa amelala nyumbani kwake akiwa na mkewe aitwaye Mekilina Mussa, lakini ghafla walitokea watu watano ambao hawafahamiki na kuvunja mlango kisha waliingia ndani ya nyumba. Inadaiwa kuwa watu hao waliokuwa wameshika mapanga, waliingia ndani ya nyumba na kuvamia chumba na kumlazimisha mke ajifunike shuka usoni na alale kitandani.
Baada ya mkewe kujifunika na shuka usoni, inadaiwa watu hao walianza kumchinja shingo Madirisha kwa kutumia panga huku mkewe akisikia jinsi mumewe alivyokuwa akilia kwa uchungu.
Kamanda Kidavashari alieleza kuwa baada ya kumchinja shingo, walichukua kichwa chake na kukiweka kwenye sufuria na kuweka maji ndani ya sufuria na kutoka nacho nje na kukipika kwenye moto ambao ulikuwa ukiwaka nje ya nyumba ya Madirisha.
Baada ya hapo, inadaiwa watu hao walirudi ndani ya nyumba na kumnyofoa sehemu za siri marehemu, mikono yake na nyayo za miguu, kisha waliziweka kwenye sufuria jingine na kuvipika kwenye moto.
Baada ya unyama huo, kwa mujibu wa madai ya Kamanda Kidavashari, watu hao waliondoka na kutokomea kusikojulikana huku wakiacha viungo hivyo vya marehemu vikiendelea kuchemka ndani ya masufuria hayo.
Kidavashari alisema mke wa marehemu baada ya kuona watu hao wametokomea, alitoka nje na kwenda kutoa taarifa kwa majirani ambao walifika kwenye eneo hilo na kukuta viungo hivyo vikiendelea kuchemka kwenye masufuria hayo, huku kiwiliwili chake kikiwa ndani ya chumba chake.
Tayari watu watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo, kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo ya kikatili

No comments:

Post a Comment