![]() |
| DC Magesa |
WAKAZI wa jiji la Mwanza jana wamekumbana na taharuki baada ya barabara
ya Nyerere kushindwa kupitika kufuatia madereva wa daladala yanayofanya safari
zake kati ya Airport, Bwiru – Igoma/Kishiri kuegesha kwenye barabara hiyo hivyo
kusababisha msongamano wa magari.Kuegeshwa kwa daladala hizo kunatokana na kutotakiwa kuegesha katika stendi
yao ya awali na badala yake kutakiwa kupitiliza yanapotoka Igoma kwenda Bwiru
ama Airport.Wakati daladala hizo zikigoma na kuziba njia katika barabara ya Nyerere,
juzi magari ya mizigo yaliziba barabara ya Pamba baada ya kuamuriwa kuondoka
katika maegesho yao ya awali ya Tanganyika kupisha wafanyabiashara ndogo
maarufu kama machinga.
Hali hiyo imesababisha msongamano wa magari kwenye barabara mbalimbali za jiji hapa wakati madereva wakitafuta njia cha mkato kuepukana na msongamano huo.Mmoja wa waathirika wa msongamano huo Odera Charles aliyekuwa akielekea Nyakato alisema amekuwepo kwenye msongamano huo kwa saa takribani nne baada ya safari yake kuishia barabara ya Nyerere akitokea Nyegezi.
Akizungumza na gazeti hili Mwenyekiti wa Madereva wa daladala, Dede Petro alisema madereva wamefikia uamuzi wa kuegesha magari yao barabarani baada ya stendi yao ya Mwaloni kugawiwa kwa wafanyabiashara ndogo ‘machinga’ na uongozi wa halmashauri ya jiji.Alisema kwa kuwa walionekana hawana thamani mbele ya jamii waliamua kufunga njia hadi muafaka uweze kupatikana baina yao na Halmashauri ya Jiji.Dede alitumia nafasi hiyo kuwaomba radhi wananchi wa jiji la Mwanza walioathirika na uamuzi wao hivyo kukosa huduma kwa zaidi ya saa 6 kwani walilazimika kufanya hivyo ili muafaka uweze kupatikana na huduma ya usafiri iweze kurejea katika hali ya kawaida.
Hali hiyo imesababisha msongamano wa magari kwenye barabara mbalimbali za jiji hapa wakati madereva wakitafuta njia cha mkato kuepukana na msongamano huo.Mmoja wa waathirika wa msongamano huo Odera Charles aliyekuwa akielekea Nyakato alisema amekuwepo kwenye msongamano huo kwa saa takribani nne baada ya safari yake kuishia barabara ya Nyerere akitokea Nyegezi.
Akizungumza na gazeti hili Mwenyekiti wa Madereva wa daladala, Dede Petro alisema madereva wamefikia uamuzi wa kuegesha magari yao barabarani baada ya stendi yao ya Mwaloni kugawiwa kwa wafanyabiashara ndogo ‘machinga’ na uongozi wa halmashauri ya jiji.Alisema kwa kuwa walionekana hawana thamani mbele ya jamii waliamua kufunga njia hadi muafaka uweze kupatikana baina yao na Halmashauri ya Jiji.Dede alitumia nafasi hiyo kuwaomba radhi wananchi wa jiji la Mwanza walioathirika na uamuzi wao hivyo kukosa huduma kwa zaidi ya saa 6 kwani walilazimika kufanya hivyo ili muafaka uweze kupatikana na huduma ya usafiri iweze kurejea katika hali ya kawaida.



No comments:
Post a Comment