KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 18, 2015

KINANA NA TIMU YAKE WAUNGURUMA WILAYA YA DIMANI MKOA WA MJINI MAGHARIBI ZANZIBAR

 Nape Nauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akiongozana na Vuai Ali Vuai Naibu Katibu Mkuu Zanzibar mara baada ya kuwasili ofisi kuu ya CCM Kiembesamaki mkoa wa Mjini Magharibi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wajumbe mbalimbali na wa wana CCM wakati alipowasili wilaya ya Kiembesamaki wilaya ya Dimani mkoa wa Mjini Magharibi jana.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Magharibi Yusuf Mohamed Yusuf akimkaribisha Ndugu Abdulrahman Kinana ili kuongea na wajumbe wa halmashauri ya wilaya ya Dimani. 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Makamu wa pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Idd mara baada ya kupokelewa katika Ofisi kuu ya CCM mkoa wa Mjini Magharibi  wilaya ya Dimani Zanzibar akiwa katika ziara ya kikazi ya siku 15 katika visiwa vya Unguja na Pemba, Katibu Mkuu Kinana anaongozana na Nape Nauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wakikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 ikiwa ni pamoja na kuhimiza uhai wa chama, Katika mkutano wa ndani akiongea na wajumbe wa mkutano mkuu wa Halmashauri ya mkoa wa  mjini Magharibi  Kinana amesema katika mambo muhimu ambayo kamati za siasa zinatakiwa kuzingatia wakati wa kuteua wagombea mbalimbali ni Maadili ya viongozi, Ameongeza kwamba kama kuna kamati ya siasa itakiuka utaratibu huo na ikaonekana kubeba baadhi ya wagombea basi Kamati Kuu  haitasitakufuata utaratibu wa kikatiba na  kuteua kamati ya siasa nyingine ili kuhakikisha haki inatendeka kwa wagombea wote walioomba uongozi.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DIMANI-MKOA WA MJINI MAGHARIBI -ZANZIBAR)

No comments:

Post a Comment