KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 31, 2015

MAMA SALMA KIKWETE AHUDHURIA MKUTANO WA KAMPENI YA KUTOKOMEZA NDOA ZA UTOTONI BARANI AFRIKA.

1
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Josephine Kulea kutoka Taasisi ya Samburu Girls ya nchini Kenya mara baada ya binti huyo kutoa ushuhuda wake kuhusu namna alivyoathirika na ndoa za utotoni wakati wa mkutano wa Marais na Wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika kuhusu kampeni ya kutokomeza ndoa za utotoni uliofanyika huko Addis Ababa nchini Ethiopia hivi karibuni. Binti huyo alijifungua mtoto wake wa kwanza akiwa na umri wa miaka 17.
2
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mke wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mama Ban Soon Taek wakati wa mkutano wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika uliozungumzia kampeni ya kupiga vita ndoa za utotoni barani Afrika wakati wa kikao cha 24 cha Umoja huo kilichofanyika Addis Ababa hivi karibuni.
3
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mke wa Rais wa Chad na Mwenyekiti wa Umoja wa Wake wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika (OAFLA) Mama Hinda Deby Itno  wakati wa kikao kilichoandaliwa na Jumuia ya Afrika kuzungumzia kampeni ya kutokomeza ndoa za utotoni barani humo hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment