Mkuu
wa mkoa wa Morogoro, Dk Rajab Rutengwe ( wa kwanza kushoto) akiwa na
Mkuu wa wilaya ya Morogoro , Said Amanzi , wakipita eneo ambalo gari la
namba SM 4151 Nissan iliyokuwa ikitumiwa na Meya wa Manispaa ya
Morogoro, Amir Nondo , ilipogongwa Januari 30, mwaka huu saa 9: 30
alasiri eneo la Mzambarauni Darajani -Msamvu barabara kuu ya Moro- Dar
na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy
Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam .Meya
huyo na watu wengine watatu walijeruhiwa na kukimbizwa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Morogoro na kulazwa wakindelea kupatiwa matibabu.
Gari la Meya likiwa halitamaniki.
Wasamalia
wakimuwahisha Hospital,Mmoja wa majeruhi mara baada ya kupata ajali
eneo la Mzambarauni Darajani -Msamvu barabara kuu ya Moro- Dar na Basi
la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy Africa
),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam .
Hili ndilo basi lililogongana na Gari ya Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo.
Meya
wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo ,(45) akiwa amelazwa wodi namba tano
ya daraja la kwanza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro
baada ya kujeruhiwa kufuatia gari yake SM 4151 ilipogongwa Januari 30,
mwaka huu saa 9: 30 alasiri eneo la Mzambarauni Darajani , Msamvu
Barabara kuu ya Moro- Dar na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba
za usajili T 831 CEH (Happy Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe
kwenda Dar es Salaam ,mbali na Meya huyo na watu wengine watatu ,Dereva
Mwambala Ally (55), na waandishi wa habari , Anita Chali (30) pamoja na
HUSSEIN Nuha (28) pia walijeruhiwa na kulazwa katika hospitali hiyo
kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
( Picha na John Nditi).
No comments:
Post a Comment