Dk Harisson Mwakyembe |
Arusha. Siku mbili baada kukabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta, waziri ambaye ameteuliwa kushika nafasi hiyo, Dk Harisson Mwakyembe amewataka Watanzania kuondoa hofu ya kuhamishwa kwake kutoka Wizara ya Uchukuzi, huku akisisitiza kuwa hana nia ya kugombea urais.
Dk Mwakyembe aliwataka wananchi kuondoa hofu kwa
sababu utendaji aliouonyesha akiwa Wizara ya Uchukuzi, atauhamishia
wizara yake mpya.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti
hili muda mfupi baada ya kuapishwa na Spika wa Bunge la Afrika Mashariki
(Eala), Daniel Kidega, Mwakyembe alisema utendaji aliouonyesha katika
wizara aliyokuwamo awali zamani, ndiyo uliomshawishi Rais Jakaya Kikwete
kumhamishia Wizara ya Afrika Mashariki ili kuongeza kasi ya utekelezaji
wa masuala ya jumuiya hiyo.
“Watanzania wanapaswa kuondoa kasumba ya kutaka
anayefanya vizuri katika nafasi yake kuendelea kubaki hapo hapo. Hapana!
Anayefanya vizuri sehemu moja ni vyema akahamishiwa sehemu nyingine ili
akafanye vizuri huko pia,” alisema Mwakyembe na kuongeza:
No comments:
Post a Comment