Rais Kiir |
Mkutano wa viongozi wa kikanda
ulioandaliwa kujadili mgogoro wa mwaka mmoja unaotokota nchini Sudan
Kusini, umecheleweshwa baada ya Rais Salva Kiir kuugua na kukimbizwa
hospitalini mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Afisa mmoja wa shirika la
IGAD, ambalo linafanya juhudi za kuwakutanisha viongozi wa Sudan Kusini
kwa lengo la kumaliza vita, aliambia BBC kwamba Rais Kiir, alianza
kuvuja damu kutoka puani
Kabla ya kuugua, hapo jana Kiir alifanya
mazungumzo na kiongozi wa waasi Riek Machar ambapo alimtaka kupuuzilia
mbali maswala yanayochochea mgogoro huo ili kumaliza mgogoro huo ambao
umedumu mwaka mmmoja
Viongozi wa kikanda, wanakutana baadaye leo, kushinikiza pande zote kufikia makubaliano ili kumaliza vita.
Swala
kuu kwenye ajenda, ni kusuluhisha maswala yanayoleta kizungumkuti
kuhusu serikali ya muungano kama moja ya suluhu la kupatikana amani.
Pande
zote zinazozozana zimekosa kufikia makubaliano kuhusu wadhifa wa waziri
mkuu na ikiwa anapaswa kuwa na mamlaka makuu au la.
Maelfu ya
watu wamefariki na wengine zaidi ya milioni moja kuachwa bila makao
tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe kuzuka nchini humo Disemba mwaka
2013.
No comments:
Post a Comment