Aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi ambaye
sasa ni Waziri wa Ushirikiano wa afriKa Mashariki Mh. Harrison Mwakyembe akizungumza na wadau mbalimbali walijitokeza katika hafla hiyo ya
kutafuta fedha za kuendesha mkutano huo utakao fanyika mapema mwezi wa
tatu.
Taasisi
ya kimataifa ya uhudumiaji wa bidhaa na uchukuzi wa bidhaa CILT yani The Chartered Institute of Logistic and Transport tawi la Tanzania imeandaa
mkutano huo mkubwa nchini ambao utafanyika katika mkoa wa Arusha tarehe 3 na
4 mwezi wa Machi lengo ni kuwakutanisha wadau mbalimbali
wa maswala ya usafirishaji na uchukuzi kujadili changamoto mbalimbli
katika sekta hiyo.
Mwenyekiti
wa CILT nchini Tanzania George Makuke akizungumza kuhusu mkutano huo na
taasisi hiyo inavyofanya kazi. Mkutano huo ambao utafanyika katika
hoteli ya Mount Meru Jijini Arusha una mipango pia ya kuwakutanisha
wanataaluma wa maswala ya uchukuzi na usafirishaji wa bidhaa ili
kubadilishana uzoefu katika taluma hiyo.
Mwenyekiti
wa kamati ya maandalizi ya mkutano huo ndugu Zakaria Hanspope akizungumza katika mkutano huo.
No comments:
Post a Comment