Mamlaka nchini Saudi Arabia kwa mara nyengine tena imeahirisha adhabu nyengine ya viboko dhidi ya mwanablogu Raif Badawi.
Hakuna sababu iliotolewa,lakini awamu mbili za kutoa adhabu kama hiyo hapo awali ziliahirishwa kutokana na sababu za kiafya.
Bwana Badawi amepewa hukumu ya viboko 1000 pamoja na kuhudumia kifungo cha miaka 10 jela kwa kutusi Uislamu.
Mwanaharakati wa Saudia ambaye pia ni wakili Suad al Shammary ambaye
alifanya kazi na bwana Badawi katika blogi yake ameachiliwa huru.
Alizuiliwa
kwa miezi mitatu bila kufunguliwa mashtaka kuhusu matamshi aliotoa
katika mtandao wa Twitter ambayo wapinzani wake walisema yanapinga
Uislamu:BBC
No comments:
Post a Comment