KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 17, 2015

TAFAKURI YA MAGGID MJENGWA KUHUSU KAULI YA NAPE NA HATMA YA PROF.MUHONGO


Ndugu zangu,
Ninapomsikiliza Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye kwenye taarifa yake inayotokana na kikao cha Kamati Kuu, Kisiwandui, naipata tafsiri moja kuu; kuwa CCM imebaini, kuwa ' Bahari Ya Kisiasa Imechafuka'.
Wimbi la Escrow ni kubwa mno kwa CCM kulidhibiti kuelekea Uchaguzi Mkuu. CCM inataka kulikwepa. Inataka kwenda kwenye uchaguzi ikiwa na sahani safi na kavu- Not only a clean slate, but a dry one.
Hivyo, CCM haina namna yeyote, bali kuwaacha wote wenye kuhusishwa na Escrow waogelee wenyewe bila kutegemea maboya ya chama. Katika hili, na kwa kupitia taarifa ile ya Nape Nnauye, Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo ametoswa rasmi.
Yawezekana kabisa kuwa Sospeter Muhongo amefanya kazi njema kwa taifa kupitia Wizara yake, lakini, maisha ya kisiasa ni magumu. Hapa hesabu za kisiasa zinamtaka aondoke, kwa kujiuzuru mwenyewe, au kusubiri kuwekwa kando na aliyemteua. Na maisha ya kisiasa yataendelea. Muhongo anaweza kurudi tena kwa nguvu zake mwenyewe.
Maggid ,
Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment