KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 17, 2015

TANGA KUNANI? BOMU LAJERUHI WATANO KWENYE BANDA LA VIDEO

Kamanda Kashai
Watu watano akiwamo mtoto wa miaka 15, wamejeruhiwa baada ya kushambuliwa kwa  bomu la mkono lililotupwa kwenye  banda la kuonyeshea picha za video.
Bomu hilo linadaiwa kuwa ni la kutengenezwa kienyeji, kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Frasser Kashai.

Kamanda wa Polisi Mkoa  akizungumzia bomu alisema ni la kurushwa kwa mkono na kwamba  lilivurumishwa juzi saa  2 usiku, kwenye kibanda cha kutizamia picha za video kilichoko  kijiji cha Amboni na kujeruhi watizamaji watano.
Waliojeruhiwa ni  Hassan Abdallah (72), Rashid Ally (45), Mrisho Abdi (29) mtoto   Juma Mtoo (15) na Abdul Ismael (19) wote wakazi wa kijiji cha Amboni.

Kashai alisema wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Tanga, Bombo wakiwa na majeraha mbalimbali mwilini na kwamba  Ally Rashid  (25) mkazi wa kijiji hicho anashikiliwa kwa uchunguzi.

Rashid anahusishwa na bomu hilo linalodaiwa ni la kutengeneza kienyeji kwa mujibu wa Kamanda.

Wakizungumzia tukio la bomu hilo, baadhi ya wananchi  waliokuwa eneo la tukio walieleza kuwa waliona kitu chenye mwanga angani  kabla ya kutua kwenye banda ambalo  walikuwemo watu zaidi ya 30 wakifurahia picha za video.

Jeshi la Polisi limewataka wananchi kutokuwa na hofu ya  tukio hilo na kwamba hali ya usalama imedhibitiwa huku uchunguzi wa kina ukiendelea na kuhimiza ushirikiano baina ya wananchi na jeshi hilo kukabiliana na uhalifu.

No comments:

Post a Comment