![]() |
| Dkt.Mwakyembe |
Rais alifanya mabadiliko kwenye baraza hilo baada
ya mawaziri wawili kuanguka kutokana na kashfa ya uchotwaji takriban
Sh306 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow.
Ikiwa imesalia miezi isiyozidi sita kabla ya
Baraza la Mawaziri kuvunjwa na akitakiwa kujaza nafasi mbili zilizoachwa
wazi na Profesa Sospeter Muhongo, aliyekuwa Wizara ya Nishati na Madini
na Profesa Anna Tibaijuka aliyekuwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Rais Kikwete alifanya mabadiliko 13, yakihusisha
mawaziri wanane na manaibu watano.
Miongoni mwa mabadiliko hayo manane ya mawaziri,
ni uhamisho wa Dk Mwakyembe kutoka Uchukuzi kwenda Afrika Mashariki huku
Samuel Sitta, ambaye aliwahi kumwelezea mbunge huyo wa Kyela kuwa ni
mmoja wa “marafiki wa kweli”, akihama kutoka Wizara ya Afrika Mashariki
kwenda Uchukuzi.
Watu wengi walioongea na gazeti hili, walisema
hakukuwa na haja ya kumhamisha Dk Mwakyembe kutokana na kazi nzuri
ambayo ameshaifanya kwenye wizara hiyo, ambayo ina tatizo kubwa la
usafiri wa reli, kuyumba kwa Shirika la Ndege (ATCL) na utendaji mbovu
kwenye bandari, mambo ambayo Dk Mwakyembe alionekana kuyashughulikia kwa
nguvu zote.CREDIT MWANANCHI



No comments:
Post a Comment