KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 26, 2015

WENGI WAHOJI MWAKYEMBE KUHAMISHWA

Dkt.Mwakyembe
 Dar es Salaam. Wasomi na wananchi kadhaa jana walizungumzia mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanywa na Rais Jakaya Kikwete, wengi wakihoji sababu za kumhamisha Dk Harrison Mwakyembe kutoka Wizara ya Uchukuzi kwenda Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Rais alifanya mabadiliko kwenye baraza hilo baada ya mawaziri wawili kuanguka kutokana na kashfa ya uchotwaji takriban Sh306 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow.
Ikiwa imesalia miezi isiyozidi sita kabla ya Baraza la Mawaziri kuvunjwa na akitakiwa kujaza nafasi mbili zilizoachwa wazi na Profesa Sospeter Muhongo, aliyekuwa Wizara ya Nishati na Madini na Profesa Anna Tibaijuka aliyekuwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rais Kikwete alifanya mabadiliko 13, yakihusisha mawaziri wanane na manaibu watano.
Miongoni mwa mabadiliko hayo manane ya mawaziri, ni uhamisho wa Dk Mwakyembe kutoka Uchukuzi kwenda Afrika Mashariki huku Samuel Sitta, ambaye aliwahi kumwelezea mbunge huyo wa Kyela kuwa ni mmoja wa “marafiki wa kweli”, akihama kutoka Wizara ya Afrika Mashariki kwenda Uchukuzi.
Watu wengi walioongea na gazeti hili, walisema hakukuwa na haja ya kumhamisha Dk Mwakyembe kutokana na kazi nzuri ambayo ameshaifanya kwenye wizara hiyo, ambayo ina tatizo kubwa la usafiri wa reli, kuyumba kwa Shirika la Ndege (ATCL) na utendaji mbovu kwenye bandari, mambo ambayo Dk Mwakyembe alionekana kuyashughulikia kwa nguvu zote.CREDIT MWANANCHI

No comments:

Post a Comment