Yanga imemburuza mahakamani mlinda mlango wao, Juma Kaseja wakitaka awalipe Sh340 milioni ikiwani fidia.
Yanga wamefikia uamuzi huo
Ijumaa iliyopita baada ya kufikisha kesi Mahakama ya Kazi na tayari
Kaseja ameshapewa notisi ya kuitwa mahakamani kujibu shtaka la kukacha
timu yake ikiwa ni pamoja na kulipa kiasi hicho cha fedha.
Yanga wanataka Kaseja awalipe
Sh340 milioni ikiwa ni ada ya usajili, ambayo ni Sh40 milioni pamoja na
fidia ya Sh300 milioni ambazo ni gharama za usumbufu wa kuvunja mkataba,
kumhudumia na kutunza kiwango chake kwa kipindi chote alichokuwa Yanga.
Mmoja wa viongozi wa Yanga
aliliambia gazeti hili kuwa kuna nyaraka ambazo Yanga wanatakiwa
kuzikamilisha ili wapangiwe hakimu wa kusikiliza kesi hiyo ambayo
itafungua ukurusa mpya wa bifu na kisasi miongoni mwa Yanga na mlinda
mlango huyo.
Wakili wa Yanga, Frank Chacha alikiri klabu
hiyo tayari imeshamfungulia mashtaka Kaseja na kesho wanategemea
kupangiwa hakimu wa kusikiliza shauri hilo.
Kaseja aliingia kwenye mgogoro
na uongozi wa Yanga baada ya Novemba 11 mwaka jana kuandika barua ya
kuvunja mkataba na klabu hiyo baada ya kukiuka makubaliano ya mkataba
kati yao akishinikiza kulipwa Sh20 milioni za usajili alizokuwa anaidai
klabu hiyo.
No comments:
Post a Comment