KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 2, 2015

GEPF WASAINI MKATABA NA BODI YA WAHASIBU NA WAKAGUZI (NBAA) WA UWEKEZAJI WA PAMOJA KATIKA ENEO LA BUNJU MJINI DAR

Mfuko wa Pensheni wa GEPF umesaini mkataba wa uwekezaji na Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) katika eneo la Bunju. Uwekezaji huo utakaohusisha kumbi za mikutano (Conference Halls) zenye uwezo wa kuchukua watu Zaidi ya 1,200, migahawa (Restaurants), Hoteli yenye hadhi ya kimataifa yenye vyumba Zaidi ya 102, Maktaba, Bwawa la kuogelea (Swimming Pool) pamoja na sehemu za mazoezi (Gymnasium) Uwekezaji huo utagharimu Zaidi ya shilingi Bilioni 10 za kitanzania na unategemewa kukamilika katikati ya mwaka huu 2015.Mkurugenzi Mkuu wa GEPF, Daud Msangi (wa pili kulia) akiongoza majadiliano ya awali kati ya Menejimenti ya GEPF pamoja na Menejimenti ya NBAA kabla ya zoezi la kutiliana saini mkataba wa uwekezaji. Mwenyekiti wa Bodi ya GEPF,Bi. Joyce Shaidi (kulia) pamoja na mwenyekiti wa NBAA Profesa Issaya Jairo wakisaini mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji wa pamoja wakiongozwa na mwanasheria wa NBAA Bi Agness Kessy. Utiaji saini huo ulishuhudiwa na makamu mwenyekiti wa NBAA Bi Anna Mbughuni ( mwenye suti ya blue), Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA Bw Pius Maneno, Mkurugenzi Mkuu wa GEPF Bw Daud Msangi pamoja na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa GEPF Bw Festo Fute. Mwenyekiti wa Bodi ya GEPF Bi Joyce Shaidi akibadilishana nyaraka za mkataba wa uwekezaji wa pamoja na Mwenyekiti wa NBAA Profesa Issaya Jairo. Pichani baadhi ya watendaji wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) wakifurahia jambo mara baada ya zoezi hilo kukamilika.

No comments:

Post a Comment