KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 1, 2015

MAGUFULI AFANYA ZIARA MBEYA

Mbunge wa Ileje Mheshimiwa Aliko Kibona akimkaribisha Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Magufuli kabla ya ukaguzi wa daraja hilo la mto Songwe.kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo Bi. Rosemary Sitaki Sinyamule.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli katikati akikata utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya Isongole-Itumba km 9 katika Wilaya ya Ileje Mkoani Mbeya. Kulia ni Mbunge wa Ileje Mheshimiwa Aliko Kibona. Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Ileje Bi Rosemary Sitaki Sinyamule, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Eng. Patrick Mfugale.
Wakazi wa Ileje wakishangilia mara baada ya Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli kuahidi ujenzi wa Barabara ya Mpemba-Isongole km 58 kwa kiwango cha lami.
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi nchini (CRB) Eng. Consolatha Ngimbwa akizungumza kuhusu usimamizi makini wa Bodi yake kwa Makandarasi kabla ya Waziri wa Ujenzi kuhutubia mamia ya wakazi wa Ileje.

No comments:

Post a Comment