KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 19, 2015

MAKONDA DC MPYA WA KINONDONI

Paul Makonda

DC Makonda, ameteuliwa kuwa mkuu mpya wa Wilaya ya Kinondoni. Kiongozi huyo wa Umoja wa Vijana wa CCM aliandikwa sana na vyombo vya habari wakati wa Bunge la Katiba kutokana na kutoa maneno ya kumshambulia mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba aliyewasilisha Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba.
Kiongozi huyo wa UVCCM aliandikwa zaidi na vyombo vya habari kutokana na kuhusishwa na vurugu zilizotokea Hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es Salaam wakati wa mdahalo wa Katiba Inayopendekezwa akidaiwa kumshambulia mwilini Warioba, ambaye amewahi kuwa Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, makada wawili wa CCM, John Guninita na Mgana Msindai walimwandikia kusudio la kumfungulia mashtaka wakidai kuwa Makonda aliwadhalilisha kwa kuwaita kuwa vibara wa Edward Lowassa, ambaye ni mbunge wa Monduli na aliwahi kuwa Waziri Mkuu.
Makonda aliwahi kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kumtuhumu Lowassa akidai kuwa anawatuma baadhi ya makada wa chama hicho wanaokivuruga chama. Alidai kuwa Lowassa hawezi kuwa Rais wa Tanzania na kwamba CCM haitafuti Rais pekee, bali mwenyekiti wake na mbunge huyo wa Monduli hawezi kuongoza chama hicho kikongwe.Rais Jakaya Kikwete ametengua uteuzi wa wakuu wa wilaya 12 na kuwateua wengine 27, akiwamo aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen na mjumbe wa Bunge la Katiba, Paul Makonda ambaye aliingia kwenye mzozo na mawaziri wakuu wawili wa zamani.
Katika uteuzi huo uliotangazwa jana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda mjini hapa, katibu mkuu wa zamani wa Shirikisho la Soka (TFF), Frederick Mwakalebela ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe, huku wakuu wa wilaya 64 wakibadilishiwa vituo vyao vya kazi.

No comments:

Post a Comment