KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 11, 2015

MKUU WA SHULE YA SEKONDARI AMKIMBIA MBUNGE WA CHADEMA

IMG_20150210_150420
Mbunge wa viti maalumu kupitia chama cha demokrasia na maendeleo chadema CHIKU ABWAO akikagua jengo lilokumbwa na ajali ya moto
……………………………………………………………………………………………………
Mbunge wa viti maalumu kupitia chama cha demokrasia na maendeleo chadema Chiku Abwao alisikitishwa na uongozi wa shule  ya sekondari ya Idodi kushindwa kumpokea kama mbunge na mama aliyeguswa na ajali ya moto katika shule kwa kuwa alikuwa ameshatoa taarifa kabla hajaenda katika shule hiyo.
Kitendo hicho kiliwafanya baadhi ya wanahabari wa manispaa ya Iringa waliokuwa wameongozana na mbunge huyo kukasirishwa na  kitendo kilichofanywa na uongozi wa shule ya sekondari ya Idodi na walianza kuhoji je? angekuwa mkuu wa mkoa,mkuu wa wilaya na waziri au mbunge wa jimbo hilo wangemfanyia hivyo.
Licha ya hujuma alizopewa ambazo zinasadikika kuwa za kisiasa mbunge wa viti maalumu kupitia chama cha demokrasia na maendeleo chadema  aliendelea na zoezi lake la kutoa msaada wa shilingi milioni moja ili kusaidia majukumu mengine ya shule hiyo kutokana tathmini fupi iliyotolewa na baadhi ya walimu.
Akizungumza mbele ya wanafunzi wa shule   Abwao amesema kuwa ameguswa na ajali hiyo ya moto ndio maana ameamua kujitolea kutoa msaada huo.
Aidha  ameishauri serikali kujenga mabweni kwa mtindo nyumba za kawaida ili kuwawezesha  wanafunzi kuishi kumi katika bweni moja tofauti na sasa ambapo wanafunzi wanaishi zaidi ya mia na ishirini katika bweni moja.
Akasisitiza kuweka ulinzi mzuri kwenye mabweni kwa kuwa suala kama hilo limekuwa likijitokeza mara kwa mara katika shule hiyo na kuomba wakandarasi watakao kuwa wanapewa tenda za kujenga mabweni ya shule kuhakikisha wanaweka vifaa maalum vya kuzimia moto.
Alipotafutwa mkuu wa shule kwa njia ya simu na kuulizwa kwanini amemkimbia mbunge alijibu  kuwa alikuwa na majukumu mengine kwa hiyo sio lazima kumpokea mbunge  na ninaweza kuwakilishwa kama kuna majukumu mengine makubwa zaidi.

No comments:

Post a Comment