KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 19, 2015

TBL YAKABIDHI MSAADA WA KISIMA CHA MAJI JIMBO LA MPENDAE,ZANZIBAR


 Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae, Zanzibar, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Uvuvi na Misitu,  Mohammed Dimwa akimshukuru Ofisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu baada ya kisima cha maji kilichochimbwa kwa msaada na TBL,  katika Jimbo hilo. Hafla hiyo Zanzibar, mwishoni mwa wiki.
 Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae na Naibu Waziri wa Uvuvi na Misitu, Said Mohammed Dimwa akimtwisha ndoo ya maji mama mkazi wa Jimbo la Mpendae, Zanzibar baada ya uzinduzi wa kisima cha maji kilichochimbwa jimbo humo kwa msaada wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). Kisima hicho kilizinduliwa mwishoni mwa wiki.
Wageni waalikwa wakinywa maji  baada ya Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae, Mohammed Dimwa kuzindua kisima cha maji kilichochimbwa kwa msaada na Kampuni ya Tanzania (TBL),  katika Jimbo hilo. Hafla hiyo ilifanyika  Zanzibar, mwishoni mwa wiki.

No comments:

Post a Comment