KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 2, 2015

TMK BINGWA WA PROIN WOMEN TAIFA CUP 2015

Waziri wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo, Mh Dkt Femella Mukangara (wa pili kushoto) akiwasili katika uwanja wa Azam Complex Chamanzi wakati wa fainali ya Mashindano ya Proin Women Taifa Cup yaliyofikia Tamati leo kwa kuzikutanisha Timu za Temeke na Pwani.
Waziri wa habari utamaduni na Michezo, Mh Dkt Fenella Mukangara akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya Temeke mara baada ya kuibuka washindi wa Mashindano ya Proin Women Taifa Cup ambayo yalichezwa katika Dimba la Azam huku Proin Promotions na Azam wakidhamini mashindano hayo.
Nahodha wa Timu ya Pwani akipokea Mfano wa hundi ya Shilingi Milioni Mbili ambazo ni zawadi ya Mshindi wa pili katika Mashindano ya Proin Women Taifa Cup na kuwamalizika kwa Temeke kuwa Mabingwa kwa kuifunga Pwani goli 1 kwa 0.
Nahodha wa Timu ya Ilala ambao ni washindi wa tatu akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni 1 ambayo mshindi wa tatu katika Mashindano hayo ni Ilala
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara (wa kwanza kulia) na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF Jamal Malinzi wakishuhudia fainali ya Mashindano ya Proin Women Taifa Cup mechi iliyochezwa katika dimba la Azam Complex kwa kuzikutanisha timu za Pwani na Temeke na Temeke Kuibuka Bingwa wa Proin Women Taifa Cup kwa kuichapa Pwani goli 1 kwa 0.

No comments:

Post a Comment