![]() |
Saada Mkuya,Waziri wa Fedha |
“Sisi hatujaona kama ni kosa kwa Watanzania kuwekeza fedha zao kwenye mabenki ya nje na wala isionekane kama ni jambo haramu kabisa.
Kama serikali tungetamani wawekeze kwenye benki nchini ili kukuza sekta ya fedha lakini pia hatuwafungi kutowekeza nje,” alisema.
“Tunachofanya ni kuiangalia hiyo ripoti ili kujua ukweli wa taarifa hizo, lakini taarifa hiyo haimaanishi kwamba ni kosa kubwa kisheria kwa Mtanzania kuweka fedha nje,” alisema.
Mkuya alisisitiza kuwa hakuna shida yoyote kwa Watanzania kuweka fedha kwenye akaunti nje ya nchi.
Waziri Mkuya ameyasema hayo siku moja tu baada ya vyombo vya habari nchini kuripoti taarifa ya kuwapo vigogo 99 wa Tanzania kuficha mabilioni ya shilingi katika benki za Uswisi kutokana na ripoti ya mtandao wa Swiss Leaks chini ya Waandishi wa Habari za Uchunguzi wa Kimataifa (ICIJ).
Taarifa ya Swiss Leaks iliyotolewa juzi Jumapili, inaonyesha kuwa vigogo hao wa Tanzania wana akaunti za siri zenye Dola za Marekani milioni 114 ambazo ni sawa na Sh. bilioni 199.6.
No comments:
Post a Comment