
Yanga watakuwa kwenye Uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya kuvaana na Tanzania Prisons ya huko, huku Azam ikipepetana na Ruvu Shooting katika Uwanja wa Mabatini, Pwani.
Kitu kinachonogesha mechi hizo ni vita ya ubingwa iliyopo baina ya Yanga na Azam, ambazo zote zinakabana koo kileleni zikiwa na pointi 25.
Lakini Azam ipo kileleni kutokana na uwiano mzuri wa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Timu hizo zitaingia dimbani zikiwa na kumbukumbu ya kufanya vizuri kwenye michezo yao ya michuano ya Afrika iliyofanyika wikiendi iliyopita, ambapo Azam iliichapa El Merreikh ya Sudan mabao 2-0 katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Yanga yenyewe ilipata ushindi kama huo wa Azam kwa kuifunga BDF XI ya Botswana kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
Vile vile kwenye michezo iliyopita ya ligi, timu hizo zilicheza na Mtibwa Sugar, ambapo Yanga ilianza kwa kuwachapa mabao 2-0, huku Azam ikiipa kisago cha mabao 5-2.
Akizungumza na MTANZANIA, Kocha Msaidizi wa Yanga, Boniface Mkwasa, alisema mechi yao dhidi na Prisons itakuwa ngumu, hivyo akawataka mashabiki wa timu hiyo kutanguliza maombi.
No comments:
Post a Comment