Na Mwandishi Wetu
BONDIA
Mtanzania Omari Kimweri anaefanya shughuli zake za mchezo wa masumbwi
nchini Australia amempiga tafu ya vifaa vya kufundishia kocha wa
kimataifa wa mchechezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'
wakati
wa zihara yake ya wiki mbili ya kutembelea nyumbani kwa ajili ya kuwapa
mabondia mbalimbali mbinu zitumiwazo na mabondia wa nje
kabla
ya hapo bondia huyo aliongea na wadau mbalimbali wa masumbwi wakati wa
mchezo wa ngumi za kulipwa kati ya Iddi Bonge na Alphonce Mchumiatumbo
mpambano uliofanyika katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba na kumvalisha mkata
wa ubingwa bondia wa uzito wa juu Mchumiatumbo baada ya kuibuka na
ushindi wa K,O ya raundi ya kwanza siku
hiyo pia alimpiga tafu kocha mkongwe wa mchezo wa masumbwi nchini
Habibu Kinyogoli kwa kumkabidhi vifaa vipya vya kufundishia mchezo wa
masumbwi.
Akizungumza
baada ya kumkabidhi vifaa kocha Super D alisema amekumbuka nyumbani kwa
kuwa ndio alipo zaliwa na kitovu chake kimezikiwa hapa nchini hivyo
ataendelea kuwakumbuka zaidi kwa kuwawezesha mabondia kucheza mara kwa
mara pindi atakapoanzisha Kimweri Promotioon itakayoshilikiana na Super D
Boxing Coach And Promotion kwa kushilikiana kuwapatia mabondia kupigana
ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kujiongezea kipato pamoja na
kupandishe rekodi zao kwa mabondia chipkizi
Naye kocha Super D alishukulu kwa kukabidhiwa vifaa hivyo ambavyo vitamsaidia kuendelea kuinua mabondia mbalimbali chipkizi.
No comments:
Post a Comment