KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 10, 2015

BREAKING NEWS! MABOMU YA MACHOZI YANARINDIMA MUDA HUU KITUO CHA MABASI UBUNGO HALI MBAYA MGOMO WA MADEREVA

Katibu wa  Madereva Mboka akiongea na wandishi wa Habari muda huu, kabla ya mabomu hayajarindima
…Mgomo wa Mabasi kuwa endelevu hadi watakapo achiwa viongozi wao wanaoshikiliwa na jeshi la Polisi
Na Andrew Chale wa Modewji blog
Modewji blog ambayo imepiga kambi katika kituo cha Mabasi Ubungo kuanzia majira ya saa 11, alfajiri, ni kuwa tayari baadhi ya viongozi wa madereva wametoa tamko  rasmi kuwa mgomo wao huo utaendelea hadi hapo viongozi wao wakuu zaidi ya Sita (6) wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi watakapoachiwa huru ikiwa ni pamoja na kuondoa masharti dhidi ya waliyowekewa katika suala la leseni kwa madereva hao.
Kwa mujibu wa Katibu Mwenezi wa madereva, Mboka Mwalaikwe alibainisha kuwa suluhu pekee kwa kunusuru abiria waendelee na safari ni kwa Jeshi la Polisi kuwaachia huru viongozi hao wanaowashikilia.
“Huu sio mgomo bali ni kueleza kwamba baadhi ya mambo wanayotufanyia Serikali sasa yamefika mwisho,  Aprili Mosi mwaka huu tulitaangaza rasmi kuwa ifikapo Aprili 10, endapo madai yetu ya msingi hayajatatuliwa basi tutagoma.
11131889_826631667373706_1365379304_n (1)
Baadhi ya madereva wakiwa wamejikusanya  muda huu huku magari yaakiendelea kuwashwa moto
Hata hivyo Jana Aprili 9, Jeshi la Polisi asubuhi limewakamata viongozi wetu sita akiwemo Mwenyekiti, msaidizi na wajumbe wake na kuwashikiria, hii bado si haki na sisi tutaendelea na mgomo huu kwanza hadi waachiwe na pia waje hapa watu wa NIT, Waziri na Jeshi la Polisi kwani wao ndio wanasababisha matatizo makubhwa” alieleza Mboka.
Kwa upande wao badhi ya madereva walioongea na Modewji blog, walieleza kuwa, wamechoka na unyanyasi unaofanywa na Serikali ikiwemo kupitia idara na taasisi zake kwani zinaanzisha mambo makubwa ambayo utekelezaji wake ni mgumu pia inawakandamiza wao madereva.
Mabomu mabomu mabomu ya machozi yanapigwa muda huu hapa standi ya mabasi Ubungo  hali ni mbaya…KWA HISANI YA MO BLOG

No comments:

Post a Comment