![]() |
Dar es Salaam. Sasa ni dhahiri kwamba polisi
wamemshika pabaya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima
baada ya kumhoji na kisha kumtaka arejee katika Kituo Kikuu cha Polisi
Dar es Salaam Aprili 16, mwaka huu akiwa na vitu 10 vinavyohusu usajili,
umiliki, uongozi na mali za kanisa analoliongoza.
Hatua hiyo imekuja kinyume na matarajio yake na ya
wengi kuwa kiongozi huyo angekuwa anahojiwa tu kuhusu matamshi yake ya
kashfa dhidi ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Dar es Salaam, Mwadhama
Polycarp Kardinali Pengo.
Kutokana na matamshi hayo yaliyosambaa kwa kasi
kwenye mitandao ya kijamii kwa njia ya video na sauti, Gwajima alitakiwa
kuripoti polisi kuhojiwa Machi 27, mwaka huu lakini kabla ya mahojiano
yao kukamilika aliishiwa nguvu na kupelekwa hospitalini alikolazwa kwa
siku nne, huku taarifa zikieleza kuwa alishtushwa na kuhojiwa taarifa
binafsi badala ya tuhuma alizoitiwa polisi.
Hata baada ya kutoka hospitalini, Gwajima
aliendelea kutembea akiwa kwenye kiti chenye magurudumu, alichotumia
hadi Aprili 6 alipohubiri katika Ibada ya Pasaka.
Siku iliyofuata askofu huyo alitupa kiti hicho
akidai kuwa amepona baada ya maombi ya wachungaji wageni waliofika
kanisani hapo kutoka Japan.
Baada ya mahojiano ya jana, wakili wake, John
Mallya alilalamikia hatua ya polisi akisema mahojiano kuchukua mkondo wa
mambo binafsi badala ya kile alichoitiwa na kusema watakwenda
kulalamikia hatua hiyo mahakamani.
|
April 10, 2015
POLISI YAMSHIKA PABAYA GWAJIMA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment