KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 10, 2015

MGOMO WA MADEREVA WA VYOMBO VYA USAFIRISHAJI WATIKISA NCHI LEO

Madereva wa Vyombo vya Usafirishaji katika maeneo mbalimbali hapa nchini, leo wameingia katika Mgomo wa kutotoa huduma hiyo, kwa kile kinachoelezwa Madereva hao kutakiwa kurudi vyuoni kwa mafunzo zaidi ya usalama barabarani.



Hali ya mgomo huo, umepelekea adha kubwa kwa abiria wa vyombo hivyo, hasa wale waliokuwa wakielekea mikoani, kwani katika Stendi kuu ya Mabasi ya Ubungo jijini Dar es salaam, hakuna basi hata moja lililoondoka huku daladala nazo zikiwa hazionekani kabisa vituoni.



Uongozi wa Madereva hao umeomba kukutana na Uongozi wa Juu Serikalini ili kulizungumzia swala hilo la kuwataka Madereva hao kurudi mafunzoni, kwani wao wanadai kuwa kazi wazifanyazo si za kudumu na hivyo watakaporudi mafunzoni hali ya maisha yao itatetereka.


Waendesha Bodaboda jijini Dar wakitembelea maeneo ya Vituo vya Daladala kuchukua abiria Baada ya Daladala kuingia katika Mgomo leo.


Wengine leo walipaga humu ili waendeleaa na shughuli zao za kila siku, maana daladala hakuna kabisa leo jijini dar.


Kituo Kipya cha Sinza ni Cheupeeeeeee....


Daladala za leo zilikuwa ni hizi, hapo ukiwa na buku mkononi unafika safari yako.KWA HISANI YA  MICHUZI BLOG

No comments:

Post a Comment