KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 6, 2015

CHUO KIKUU HURIA CHATAKIWA KUWA NA UBUNIFU WA MAPATO

01
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria  cha Tanzania Prof Tom Mbwete akitoa neno la shukurani  Mkoani Katavi  wakati wa hafla fupi ya kuagwa na wanafamilia wa Chuo hicho tawi la Mkoa wa Katavi katika Hafla
 
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Ibrahimu Msengi ameshauri  Uongozi wa Chuo Kikuu Huria tawi la Mkoa wa Katavi kuwa wabunifu katika kutafuta vyanzo vya mapato kuliko kutegemea Ada ya wanafunzi  na ruzuku ya serikali  katika  kujiendesha kuliko kutegemea pato moja tu ambalo ni ada ya wanachuo.
Ametoa rai hiyo wakati akihutubia Jumuiya ya wananchuo na wananchi waliofurika kwenye ukumbi wa chuo hicho kwa ajili ya kumuaga Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof,Tom Mbwete aliyemaliza muda wake kukiongoza chuo hicho.  na  sasa anakwenda kuhudumia maeneo mengine katika nchi za Bara la Afrika.
Dkt Msengi amesema uongozi wa Chuo Kikuu Huria  Mkoani humo utumia fursa zilizopo katika Mkoa  kuhakikisha wanakuwa wabunifu kupata  vyanzo vya mapato,ambapo wamepata eneo la kujenga Chuo akashauri waweke miundo mbinu itakayoasaidia kukiingizia chuo mapato kama kujenga kumbi kubwa zitakazotumika  kwa ajili ya mikutano  mbalimbali,pamoja na kumbi za semina kwa wanafunzi ,na pengine watu kutoka nje wanaweza kuja kukodisha na kuweza  kukiingizia Chuo  mapato.
iliyofanyika kwenye ukumbi wa Chuo hicho
02
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Ibrahim Msengi  katikati anayefuatia kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania aliyemaliza muda wake akibadilishana mawazo na Viongozi wa Mkoa  wa Katavi wakati wa hafla ya kumuaga iliyofanyika kwenye ukumbi wa Chuo hicho mjini Mpanda.               

No comments:

Post a Comment