Serikali ya Kenya imemtambua mmoja
ya wapiganaji waliohusika katika mauaji ya chuo kikuu cha Garissa kwamba
ni mtoto wa afisa wa serikali.
Msemaji wa wizara ya ndani amesema
kuwa Abdirahim Abdullahi ni miongoni mwa watu wanne walioshambulia chuo
kikuu cha Garissa siku ya alhamisi na kuwaua watu 148.
Mtu huyo sasa ametambulika kama mwana wa kiume wa Chifu wa eneo la Kazkazini mashariki mwa kenya.
Alidaiwa kutoweka na ilihofiwa kwamba amesafiri nchini Somalia.
Wizara ya ndani inasema kuwa wapiganaji wote waliuawa siku ya alhamisi.
Washukiwa
wengine watano wamakamatwa kufikia sasa kwa kuhusishwa na mauaji hayo
ambayo ni mabaya zaidi kuwahi kutekelezwa na kundi la wapiganaji wa
Alshabaab.-BBC


No comments:
Post a Comment