KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 8, 2015

SERIKALI KUDHIBITI MATUMIZI MABAYA YA TEHAMA.



 Makamu Mkuu wa Chuo cha Bagamoyo.Profesa Costa Mahalu akizungumza na waandishi wa habari leo juu ya utumiaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) katika semina iliyofanyika leo katika hoteli ya New Afrika,Jijini Dar es Salaam.Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi,Teknolojia na Mawasiliano,Profesa Patrick Makungu akizungumza na waandishi wa habari leo juu ya utumiaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) katika semina iliyofanyika leo katika hoteli ya New Afrika,Jijini Dar es Salaam.Meneja Mradi wa Idara ya Uchumi na Mendeleo ,Mazingira na Utalii wa Afrika Kusini,Rolda Rapotu akizungumza na  katika semina ya wadau wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano iliyofanyika  leo katika hoteli ya New Afrika ,Jijini Dar es Salaam.PICHA NA EMMANUEL MASSAKA
=========  ==========  ===========
 Wizara ya Sayansi,Teknolojia na Mawasiliano imesema itaendelea kudhibiti matumizi ya mtandao katika kuhakikisha hayatumiki vibaya kwa watumiaji.
Hayo ameyasema leo Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi,Teknolojia na Mawasiliano,Profesa Patrick Makungu wakati wa Semina ya Maendeleo ya Jamii na Utumiaji Teknolojia ya Habari na Mawasiliano iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya New Africa,Jijini Dar es Salaam. Makungu amesema kuwa Wizara ya Sayansi,Teknolojia na Mawasiliano imepitisha sheria ya matumizi ya mitandao katika kulinda ili kulinda matumizi hayo yasitumike vibaya na kuharibu sura ya nchi.Amesema kuwa tafiti mbalimbali za mitandao  zimeanza 2010 hali ambayo zinaendelea na kufanya hivyo itasaidia nchi kupata maendeleo katika sekta ya mawasiliano. Naye Mratibu wa Semina ya Maendeleo ya Jamii na Utumiaji Teknolojia ya Habari na Mawasilino,Profesa Benson Nindi amesema kuwa wanaufanya mradi huo katika suala zima la kutoa elimu juu ya utumiaji wa mitandao na serikali ya Tanzania inatakiwa kutunga sera ambayo itasaidia wananchi kwenda kasi na teknolojia ya habari na mawasiliano.

No comments:

Post a Comment