KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 4, 2015

UKWASI WA ZIITO HADHARANI


 



zittoNa Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
UKWASI wa Kiongozi Mkuu wa Chama Cha Alliance for Change and Transparency(ACT Wazalendo), Zitto Kabwe umeongezeka kutoka umiliki wa shamba moja na Sh milioni 30 alizokuwa amezihifadhi katika akaunti za benki mbili tofauti hapa nchini, na sasa anamiliki mali na fedha zinazofikia Sh milioni 690, MTANZANIA Jumamosi linaripoti.
Kwa mujibu wa taarifa hizo mpya alizoziweka hadharani wiki hii katika fomu maalum ya kuonyesha mali zinazomilikiwa na viongozi wa chama hicho, Zitto ametanabaisha kuwa kwa sasa anamiliki nyumba mbili.
Nyumba hizo, moja ina thamani ya Sh milioni 180 na nyingine Sh milioni 43, Pia anamiliki kitalu cha ekari 12 ambacho kinathamani ya Sh milioni 25, vyote vikiwa Mwandiga mkoani Kigoma.
Zitto pia ameweka hadharani kumiliki mashamba matatu katika mikoa ya Kigoma, Mtwara na Dar es Salaam.
Katika ufafanuzi wake kuhusu mashamba hayo, Zitto ameeleza kuwa anamiliki shamba la ekari sita katika manispaa ya mji wa Mtwara likiwa na thamani ya Sh milioni 60.
Hali kadhalika shamba lingine la ekari tatu lenye thamani ya Sh milioni 20 huko Matyazo Kigoma, lingine la ekari 3 lenye thamani ya shilingi milioni 90 ambalo liko Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Katika fomu hiyo, Zitto alijaza kuwa anamiliki pia gari moja aina ya Land Lover, Free Lander ambalo alinunua kwa dola za Kimarekani 40,000 sawa na Sh. milioni 72.
Kwa upande wa fedha alizokuwa nazo wakati anajaza fomu hiyo ni Sh. milioni 18, pia alitanabaisha kuwa amehifadhi fedha katika Benki ya CRDBNMB na STANBIC zenye jumla ya Sh milioni 9.8.HABARI ZAIDI SOMA  MTANZANIA

No comments:

Post a Comment