KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 7, 2015

WAANDISHI ZANZIBAR WAKAMIA KUPAMBANA JUU YA HAKIZA WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI

unnamedNa Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
…………………………………….
Waandishi wa habari nchini wameazimia kuboresha Fani ya Uandishi na Utayarishaji wa Vipindi Vinavyohusu Watu wenye Ulemavu wa Akili ili kuzidi kutetea Maslahi na Haki za Watu hao.
Maazimio hayo wameyatoa katika Semina ya Siku mbili ya kuwajengea Uwezo waandishi hao iliyoandaliwa na Jumuiya ya Watu wenye Ulemavu wa Akili Zanzibar (ZAPDD) kwa Msaada wa Mwenvuli wa Asasi za Kiraia.
Wamesema kuna kila haja ya kuboresha Habari na Vipindi wanavyotoa kutokana na Jamii ya Watu wenye Ulemavu wa akili kukumbwa na Changamoto nyingi na hivyo kukoseshwa haki zao za Msingi.
Aidha wameazimia kuongeza Ushirikiano wa karibu baina yao na Jumuiya ya ZAPDD ili kuona Jamii hiyo inawezeshwa kama zilivyokuwa jamii nyingine nchini.
Awali akitoa mada katika Semina hiyo Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu Ally Uki aliwataka Wanahabari hao kuwasaidia Walemavu hao wa Akili kwa kufichua maovu wanaotendewa ili Jamii ipate uelewa na kulinda haki zao.

No comments:

Post a Comment