KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 3, 2015

WAZIRI WA FEDHA SAADA MKUYA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA BANDARI KAVU

1
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya akiangalia kontena lenye shehena ya vitenge badala ya unga wa gypsum kama nyaraka zilivyoonyesha.
4
Baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  na wa  bandari kavu wakihakiki vitenge vilivyotolewa katika makontena.
5
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya pamoja na Kamishna wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Tiagi Kabisi wakipitia kwa makini nyaraka za vifaa hivyo.
16
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya akiongea na simu katikati ya runinga zilizoshushwa katika kontena.
17
Kamishna wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Tiagi Kabisi akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari.                   
Baadhi ya wafanyabiashara wabainika kukwepa kulipa kodi kwa kuingiza bidhaa kutoka nje kupitia bandari ya Dar es Salaam, ambapo huandikisha taarifa na maelezo tofauti na bidhaa halisi zilizomo ndani ya makontena ili kuwawezesha kukwepa kodi kwa kulipia kiasi kidogo.
Kutokana na udanganyifu huo, Waziri wa Fedha Mh. Saada Mkuya alifanya ziara ya kushtukiza katika bandari kavu Karibu na BP Kurasini jijini Dar es Salaam na kubaini kuwepo kwa makontena nane yenye bidhaa tofauti na zilizoandikishwa kwenye nyaraka. Bidhaa zilizokutwa kwenye makontena hayo ni pamoja na Vitenge pamoja na  Vifaa vya  kutengenezea pikipiki. Mhe. Waziri wa fedha vilevile alifanya mshtukizo huo kwa siku mbili ambapo siku ya pili alishtukiza bandari kavu ambayo ni TRH iliyoko kurasini .Huko aligundua kuwa waliweka Luninga na Biskuti katika makontena yenye ukubwa wa futi 40 kila moja.
                        

No comments:

Post a Comment