Waziri Sitta |
Madereva hao jana walitoa tamko la kuwapo kwa mgomo huo kupitia
vyama vyao, huku wakikanusha kwamba watagoma sambamba na kuandamana.
Walisema leo watakuwa kwenye ofisi zao za muungano wao zilizopo Ubungo, jijini Dar es Salaam na hawatatoa huduma za usafiri.
Akizungumza na NIPASHE jana, Katibu wa Umoja wa Madereva na Chama
cha Malori, Rashid Salehe, alisema, mgomo upo pale pale kwa madai kuwa
bado kuna mambo ambayo yameendelea kuwa kikwazo kwao.
Alisema iwapo serikali haitatoa majibu ya kuridhisha, leo hawataingia barabarani kutoa huduma za usafiri.
Alisema jana walifanya mkutano wa madereva jijini Dar es Salaam huku ajenda kubwa ikihusu mgomo huo.
Alitaja baadhi ya sababu zinazowafanya wagome kwa mara nyingine
kuwa ni serikali kutotekeleza madai yao likiwamo la kupewa ajira rasmi
na waajiri wao.
“Msimamo wetu upo palepale kwamba kesho (leo) hatutaendesha
magari..madereva wanaambiwa wezi, tunataka mikataba iboreshwe…tutakaa
hapa hata ndani ya siku saba hadi serikali ije na kutoa majibu
yanayoridhisha. Tunataka tupatiwe mikataba inayoeleweka na waajiri wetu
mbele ya serikali,” alisema na kuongeza:
“Tumekaa katika kikao cha leo (jana) kwa ajili ya kuangalia
maazimio ya kikao tulichokaa Aprili 29, mwaka huu…katika kikao hicho
zaidi ya madereva 40 walisema hawana hela.”
No comments:
Post a Comment