RAIS KIKWETE ATOA MSAADA KWA TIMU YA MICHEZO KILIMANI MJINI DODOMA
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiikabidhi timu ya soka ya Kilimani Sports
Club jezi na mipira katika ikulu ndogo ya mjini Dodoma leo asubuhi.Rais
Kikwete alitoa msaada kwa timu hiyo baada ya kuwakuta vijana hao
wakifanya mazoezi bila zana bora katika uwanja wa mpira ulioko eneo la
Kilimani karibu na ikulu wakati Rais alipokuwa akifanya mazoezi ya
kutembea katika eneo hilo.Wakiongea mara baada ya kupokea msaada huo
vijana hao walimshukuru Rais Kwa moyo wake wa upendo na nia yake ya
kukuza vipaji kwa vijana na kuahidi kufanya vyema katika ligi ya Wilaya
ya Dodoma mjini.
No comments:
Post a Comment