KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 25, 2015

VYAMA VYA UPINZANI VYASUSIA MAZUNGUMZO NCHINI BURUNDI

Picha inayoonyesha taswira ya Burundi

Vyama vya upinzani katika mji mkuu wa Burundi vimesimamisha mazungumzo na  serikali kupinga kuzorota kwa usalama baada ya mauaji kiongozi wa upinzani, Zedi Feruzi, Bujumbura, Burundi.
               
Burundi iko kwenye mgogoro mkubwa kutokana na maamuzi ya Rais Pierre Nkurunziza kuwania awamu ya tatu ya Urais sanjari na jaribio la mapinduzi  lililoshindwa mapema mwezi huu. 

Viongozi wa upinzani wanasema wanasitisha mazungumzo na serikali ya Nkurunzinza." Hatuiwezi kuendelea kuzungumza wakati kuna vitisho na mauaji," anasema Pacifique Nininahazwe, mmoja wa wanaharakati.

Muendelezo wa machafuko.

Kiongozi wa upinzani Feruzi, aliuawa na watu wenye silaha juzi akiwa pamoja na mlinzi wake.

Siku moja kabla, watu watatu waliuawa  na wengine 21 walijeruhiwa kutokana na mlipuko wa makombora sokoni.

Wiki iliyopita, Rais Nkurunziza alishinikizwa umoja wa mataifa kusimamisha uchaguzi baada ya ma.andamano hayo,alisogeza uchaguzi kwa siku 1o.

No comments:

Post a Comment