KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 26, 2015

JINO KWA JINO YAANZA TENA ZANZIBAR

Mgogoro wa kisiasa Zanzibar umeingia katika hatua nyingine baada ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukataa hoja ya Spika wa baraza hilo ya kumwalika Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, kuhudhuria kuvunjwa kwa baraza hilo leo.
Hali hiyo inaashiria kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaiaf (SUK) iliyoundwa na Chama cha Wananchi (CUF) na CCM baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 imepata majaribu.
Awali akitoa taarifa katika kikao cha Baraza la Wawakilishi jana, Spika wa baraza hilo, Pandu Ameri Kificho, aliwataarifu wajumbe hao kuwa wakati wa kuvunjwa kwa baraza hilo wageni watatu wanatarajiwa kuhudhuria akiwamo Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu, Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif na mlinzi wa rais.
Hata hivyo, Kificho alisema wajumbe wa baraza hilo ndiyo wenye mamlaka ya kukubali au kukataa wageni hao kuhudhuria na kutaka idhini yao.
Spika huyo alipowauliza wajumbe hao kama  wanakubaliana na ujio wa wageni hao, wajumbe hao kwa kauli moja walimjibu kuwa Jaji Mkuu wa Zanzibar na mlinzi wa Rais wa Zanzibar wanamruhusu kuingia lakini walikataa Makamu wa Kwanza wa Rais (Maalim Seif) asiingie katika kikao hicho.
SPIKA: Ndugu wajumbe wageni wetu wakuu kesho (leo) ni watatu na tayari nimeshawapelekea barua ya kuwaalika kuhudhuria katika ufungaji wa kikao hiki, nataka kauli zenu vipi bodigadi wa rais mnamruhusu?.
WAJUMBE: Ndiyooo
SPIKA: Je?, Jaji Mkuu wa Zanzibar mnamruhusu?
WAJUMBE: ndiyoooo
SPIKA: Mgeni wetu mwengine ni Makamu wa Kwanza wa Rais vipi mnamruhusu?
WAJUMBE: Hatumtaki.
Spika Kificho alirudia kuuliza mara tatu swali hilo lakini majibu ya wajumbe mara zote yalikuwa ni hayohayo ya kumkataa Maalim Seif kuhudhuria.
Kufuatia hali hiyo, Kificho aliwaambia wajumbe hao kama hawataki Makamu wa Kwanza wa Rais kuhudhuria kikao hicho kwa kuwa alishamwandikia barua ya mwaliko itabidi amwandikie tena barua ya kumtaarifu kongozi huyo kuwa asihudhurie kikao hicho kutokana na wajumbe wa baraza hilo kukataa ujio wake.
Baadhi ya wajumbe wa CCM wakizungumza na NIPASHE, walieleza sababu za kukataa Maalim Seif kuhudhuria shughuli hiyo.
Kaimu Mnadhimu wa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka CCM, Ali Salum Haji, alisema wana sababu za msingi kukataa Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF kuhudhuria kikao hicho, ikiwamo kuwa yeye ni kiongozi wa upinzani lakini wajumbe wake na mawaziri wa chama chake wamesusia baraza hilo. CHANZO:NIPASHE

No comments:

Post a Comment