KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 23, 2015

KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YAKE KATIKA MAONYESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA

Afisa wa Jeshi la Magereza nchini, Nsajigwa Mwankenja akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil kuhusu shughuli zinazofanywa na Jeshi hilo, wakati Katibu Mkuu alipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakati wa maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil, akipata maelezo kutoka kwa Maafisa wa Uhamiaji kuhusu shughuli zinazofanywa na Idara hiyo, wakati alipotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akisoma vipeperushi vya Idara ya Uhamiaji wakati alipotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment