KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 19, 2015

KIKWETE AKABIDHIWA MAGARI 50 YA WAGONJWA

Rais Jakaya Kikwete.
RAIS Jakaya Kikwete            
                          
RAIS Jakaya Kikwete amekabidhiwa jumla ya magari ya kubebea wagonjwa 50 kutoka kwa kampuni ya vito ya Decent Dia Jewel (DMCC), yenye thamani ya Dola za Marekani 300,000 kwa ajili ya kusambazwa maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza baada ya kukabidhi funguo za magari hayo, Mwenyekiti wa kampuni hiyo, Chetan Shah alisema magari hayo yatasafirishwa na kuwasili rasmi nchini kuanzia mwezi Julai mwishoni hadi Agosti.

“Tunakukabidhi magari haya ya kubeba wagonjwa kwa ajili ya kusambazwa maeneo mbalimbali, ikiwemo vijijini. Wazo la kutoa msaada huu nililipata nilipotembelea Tanzania na kushuhudia namna wananchi hasa wa vijijini walivyokuwa wakitaabika kwa kukosa huduma za afya kutokana na ukosefu wa usafiri,” alisema Shah.

Alisema amekuwa akitembelea Tanzania mara kwa mara hasa kutokana na biashara ya kampuni yake ya madini na ndipo alipopata uamuzi wa kutoa magari hayo kusaidia wale wote wasio na uwezo wa usafiri katika sekta ya afya.

Kwa upande wake, Rais Kikwete aliishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo na kukiri kuwa bado kuna maeneo nchini yenye uhitaji mkubwa wa magari ya wagonjwa. “Hili ni eneo ambalo ki ukweli bado lina uhitaji mkubwa.

Tunashukuru sana kwa kufikiria kutusaidia na kwa kweli msaada huu utatufaa sana,” alisema.CHANZO HABARI LEO

No comments:

Post a Comment