KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 27, 2015

KINANA ATAHADHARISHA WAGOMBEA KUWA MAKINI NA WAPAMBE

Katibu mkuu wa Chama Cha  Mapinduzi (CCM ) Abdulrahman Kinana,  amewatahadharisha makada wa chama hicho wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi kuwa makini na watu wanaojiita wapambe kwani wapo  kwa ajili ya maslahi ya kifedha.
 
Kinana aliyasema hayo jana kwenye mkutano wa ndani wa halmashauri ya jimbo la Sumve wakati akizungumza na wajumbe wa chama hicho, wilayani Kwimba mkoani Mwanza.
 
Kinana alisema kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi hivyo ni vyema wagombea wakachukua tahadhari juu ya watu hao ambao ni wapiga debe wa watangaza nia ili kuwawezesha kupata nafasi ya uongozi.
 
"Kuweni makini na hawa wajanja wanaojiita wapambe au wapiga debe, kwa maana wapambe wengine mbali na kuujua ukweli kwamba wananchi hawakukubali lakini bado anakula fedha zako bila kuwa na wasiwasi tena akizidi kukupa matumaini hewa," alisema Kinana.
 
Alisema, maeneo mengi wagombea wameumizwa na wapambe hao hivyo ni vema  kuwa makini na kuchukua tahadhali katika hilo.
 
Aliwasihi Watanzania kuchagua viongozi wa  CCM kwani ndiyo viongozi bora wanaojua matatizo ya wananchi.
Kinana alisema kuwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, aliwahi kusema kuwa viongozi ni wengi, lakini kiongozi bora atatokana na Chama cha Mapinduzi.
 
Kinana anaendelea na ziara yake ya kukagua, kuhimiza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wa  CCM 2010/15 mkoani hapa pamoja kuhimarisha chama hicho. 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment