KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 27, 2015

NAPE 'AZIMA' MGOGORO WA UHURU PUBLICATIONS

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amezima mgogoro ndani ya magazeti ya Uhuru na Mzalendo yanayomilikiwa na chama hicho kupitia kampuni ya Uhuru Publications.
Hatua hiyo ilifikiwa jana jijini Dar es Salaam baada ya Nape kufanya mazungumzo na wafanyakazi hao.
Wafanyakazi wa magazeti hayo walishiriki mgogoro huo uliohusishwa na masuala ya siasa, chanzo chake kikitajwa kuwa ni hatua ya Bodi ya kampuni ya Uhuru Publications kufanya mabadiliko ya uongozi wake na kumbadilishia kazi Mhariri Mtendaji wake, Joseph Kulangwa.
Nape alimthibitishia mwandishi wetu kushiriki kwake kikao na wafanyakazi wa kampuni hiyo, huku akisisitiza kuwa baada ya mazungumzo, pande zote zilielewana na mgogoro huo kumalizika.
Hatua zilizofikiwa na bodi ya kampuni hiyo, licha ya kumbadilishia kazi Kulangwa, iliwabadilisha kazi watendaji wengine watatu wa idara ya biashara,  ukaguzi na rasilimali watu kuanzia Jumanne iliyopita.
Taarifa za ndani zilieleza kuwa Kulangwa ambaye awali alikuwa mwajiriwa wa magazeti ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayomilikiwa na serikali, alishika wadhifa huo miezi 13 iliyopita.
Kuhusu mtikisiko wa kiuchumi ulioikabili kampuni hiyo, inaelezwa kuwa sekretatieti ya CCM chini ya Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana, ilitoa zaidi ya Shilingi milioni 400 katika kulipa madeni ikiwamo uchapaji na ulipaji mishahara kwa wafanyakazi wa Uhuru.
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment