KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 27, 2015

SERIKALI YAONDOA MUSWADA WA HABARI BUNGENI

Prof.Mwandosya
Hatimaye serikali imeondoa Muswada wa Sheria ya Haki ya upatikanaji habari wa mwaka 2015, uliokuwa usomwe kwa mara ya pili leo na badala yake utasomwa katika Bunge la kwanza la serikali ijayo. 
 
Akitoa taarifa ya kuondolewa kwa Muswada huo jana bungeni, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Mark Mwandosya, alisema Muswada huo ulichapishwa Februari 20, 2015 na kusomwa kwa mara ya kwanza bungeni Machi 12, hadi Aprili Mosi, mwaka huu.
 
"Mheshimiwa Naibu Spika huu si muswada wa dharura kama ambavyo wengine wanazungumza,"alisema.
 
Alisema kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, iliyokutana Juni 22, mwaka huu ilijadili kwa kina Muswada huo na kuzingatia maoni ya wadau wa tasnia hiyo na kushauri kuwa inahitaji muda zaidi kuujadili na kuendelea kupata maoni zaidi ya wadau.
 
"Serikali imetafakari maoni ya kamati na kuafiki muswada uendelee kufanyiwa kazi hadi hapo kamati itakapokamilisha kazi yake ipasavyo na kuwakilisha maoni yake bungeni,"alisema.
 
Alisema matarajio ni kwamba muswada huo utasomwa kwa mara ya pili na ya tatu katika bunge lijalo.
 
Juni 22, mwaka huu, wadau mbalimbali wa habari, waliokutana mjini Dar es Salaam  walipinga muswada huo, kwa kile kinachoelezwa kuwa unakiuka sheria za kimataifa, Katiba ya nchi na kuwanyima haki raia kupata taarifa na kuua ndoto ya vijana wanaotarajia kunufaika na tasnia ya habari.
 

No comments:

Post a Comment