KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 25, 2015

WAANDAMANA NJE YA UBALOZI WA UINGEREZA KIGALI KUPINGA KUKAMATWA KWA JASUSI WA RWANDA

Protesters calling for the release of General Karenzi Karake outside the British High Commission in Kigali, Rwanda on 24 June 2015. 
Watu 200 wamekusanyika nje ya  ubalozi wa Uingerenza  jijini Kigali nchini Rwanda  kupinga kukamatwa kwa  Jen Karenzi Karake nchini Uingereza 

Jen Karake 54, alikamatwa uwanja wa ndege  wa Heathrow kwa  tuhuma za mauaji ya kimbari , Jen Karake, 54, alishikiliwa uwanja wa ndege  jumamosi ,akituhumiwa kuamuru mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 .

Waandamanaji wametishia  kutosimamisha maandamano nje ya ubalozi katika mji mkuu wa Kigali hadi atakapo hachiwa huru,atafikishwa kortini leo.

Serikali ya Rwanda imechukulia kukamatwa kwake kama" upuuzi"Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda  Louise Mushikiwabo amelaumu kushikiliwa kwa Jen Karake na kusema kuwa  "mshikamano wa ulaya kuikandamiza Afrika haukubaliki

Mwakilishi wa BBC Afrika mashariki  Karen Allen anasema kuwa  kauli ya waziri huyo imechochea maandamano hayo ya jana

"Tuko hapa tukishikamana  na mashuja wetu  ambao walikuwa miongoni mwa waliosimamisha mauaji ya kimbari nhini mwetu,'' anasema Herbert Muhire,mmoja wa waandamaji

Balozi wa Uingereza nchini Rwanda ,William Gelling, kwa ufupi aliwahutubia waandamanaji na kusema;

"Naweza kusema kuwa  haya ni  maamuzi ya  sahihi ya kisheria kama mnavyoelewa ...Uingereza ni mshirika wa karibu wa Rwanda 

No comments:

Post a Comment