KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

July 28, 2015

JIVUNIENI UTANZANIA WENU, JIVUNIENI LUGHA YA KISWAHILI- KATIBU MKUU MULAMULA


Katibu Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
Katibu Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Mkuu wa Utawala, Bi Lilian Munanka, ambaye Balozi amemwelezea kama Afisa Mkuu Mwandamizi, mweledi, mchakapakazi, anayejituma na mwajibikaji, mwenyeuzoefu mkubwa na nguzo ya kutegemewa na ambaye amewapokea Mabalozi wengi.
Katibu Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula akiwa na baadhi ya maafisa na wafanyakazi wa Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa wakiongonzwa na Balozi Ramadhani Mwinyi.

Katibu Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula, amewaaga watanzania waishio nchini  Marekani,  kwa kuwataka kujivunia utanzania wao na kutoionea aibu lugha yao ya taifa,   Kiswahili.

Mwishoni mwa wiki,   Ubalozi wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania nchini Marekani,  uliandaa hafla ya aina yake  ya  kumpongeza, kumshukuru na kumuaga  Balozi Liberata  Mulamula ambaye sasa ni  Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

No comments:

Post a Comment