Katibu
Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi
Liberata Mulamula akiwa na Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa
Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
Katibu
Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi
Liberata Mulamula akiwa na Mkuu wa Utawala, Bi Lilian Munanka, ambaye
Balozi amemwelezea kama Afisa Mkuu Mwandamizi, mweledi, mchakapakazi,
anayejituma na mwajibikaji, mwenyeuzoefu mkubwa na nguzo ya
kutegemewa na ambaye amewapokea Mabalozi wengi.
Katibu
Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi
Liberata Mulamula akiwa na baadhi ya maafisa na wafanyakazi wa
Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa wakiongonzwa na
Balozi Ramadhani Mwinyi.
Katibu
Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi
Liberata Mulamula, amewaaga watanzania waishio nchini Marekani, kwa
kuwataka kujivunia utanzania wao na kutoionea aibu lugha yao ya taifa,
Kiswahili.
Mwishoni
mwa wiki, Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini
Marekani, uliandaa hafla ya aina yake ya kumpongeza, kumshukuru na
kumuaga Balozi Liberata Mulamula ambaye sasa ni Katibu Mkuu, Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
No comments:
Post a Comment