KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

July 28, 2015

PSPF NA MAX MALIPO WAUNGANA KUKOMBOA WAJASIRIAMALI

Na Benjamin Sawe,Maelezo

Mabadiliko katika sekta ya hifadhi ya jamii nchini yamepelekea kuwepo na mabadiliko ya sheria ya mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma (PSPF). Sheria ya Mfuko wa pensheni wa PSPF sasa inaruhusu kusajili wanachama katika sekta zote za umma na binafsi. Na kwa sasa mfuko una mipango miwili ya uchangiaji wa lazima yaani PSPF Mandatory Scheme na mpango wa uchangiaji wa hiari yaani PSPF Supplementary Scheme

Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwandishi wa Makala hayaBi Mwanjaa Sembe, Meneja Mpangowa Uchangiaji wa Hiari PSPF anasema uwasilishaji michango kwa kutumia huduma ya MaxMalipo itawasaidia wachangiaji kupata huduma za michango yao.

Anasema huduma ya kulipia kupitia mfumo wa Maxmalipo imeanzishwa na mfuko wa pensheni wa PSPF kwa ajili ya kupanua wigo kwa wanachama wa mfuko huo kuchangia na kujua salio la michango yao popote walipo ambapo huduma hiyo itawarahisishia watumiaji kutosafiri kwa umbali mrefu ili kupata huduma hiyo.
Mfuko umeona adha na shida walizokuwa wanazipata wateja wetu ndio maana tukaamua pamoja na huduma nyingine zitolewazo na mfuko wetu tujiunge na wenzetu wa Kampuni ya MaxCom inayotoa huduma ya Max Malipo ili kuweza kuwakomboa wateja waweze kuchangia pamoja na kujua kiasi cha michango yao kwa urahisi kwa kutumia huduma hiyo hivyo kuwafanya kuwa na muda mrefu wa kutafuta kipato badala ya kusafiri kwa umbali mrefu kufuata huduma.Anasema Bi. Sembe.

Anasema masuala ya hifadhi ya jamii yanagusa kiini muhimu sana cha wafanyakazi kwenye sekta rasmi na sekta zisizo rasmi hasa za watu masikini pamoja na sekta ya bima za jumuiya za waajiri.

Uchunguzi unaonyesha kuwaIdadi kubwa ya watu waliomo katika mifuko hii ya hifadhi ya jamii ni wale ambao wameajiriwa kwenye sekta iliyo rasmi. Hifadhi ya jamii ni haki ya kila mtu ndiyo maana mfuko wa pensheni wa PSPF wana mpango wa uanachama wa hiari kama mkakati wa makusudi juu ya kupanua wigo wa hifadhi ya jamii ili kuhakikisha ya kuwa hata wale waliojiajiri kujiunga na mfuko wa PSPF na hata wale wanachama wa mifuko mingine iliyopo kuweza kuweka akiba ya ziada.

No comments:

Post a Comment