KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

July 27, 2015

KAMPUNI YA TIGO TANZANIA KUSAMBAZA SIMU ZA SMARTPHONES WAKATI WA MAONESHO YA NANENANE

go1
Meneja wa mawasiliano wa Tigo Tanzania, John Wanyancha akiongea na wanahabari(hawapo pichani) wakati wa kutangaza udhamini wa Tigo kwenye maonesho ya Nane nane kitaifa mwaka huu, kushoto ni mwenyekiti wa TASO, Engelbert Moyo.
…………………………………………………..

Wakulima na wageni mbalimbali watakaoshiriki kwenye maonesho ya nanenane ya mwaka huu wanatarajia kupata punguzo la bei ya simu za smartphones kutoka Tigo katika jitihada za kampuni ya mawasiliano ya simu kuwapatia watanzania wengi iwezekanavyo kupata kufurahia mambo ya kimtandao.

Akitangaza ushiriki wa Tigo katika maonesho ya  nanenane ya  mwaka huu kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam leo, meneja mawasiliano wa Tigo Bw. John Wanyancha alisema, gharama nafuu za smartphones ni sehemu ya lengo la kampuni la kukuza mabadiliko ya maisha ya kidijitali kwa kuwapa watanzania upatikanaji wa mtandao wa intaneti  kupitia simu zao za mkononi.

Lengo letu ni kuwafanya watu waujue ulimwengu, ulimwengu ambao una fursa za kijamii na kiuchumi zisizokuwa na kikomo. Tunawahimiza wageni watakaotembelea maonesho ya nanenane kupita kwenye banda la Tigo ili kujionea bidhaa zetu mbalimbali za kidijitali na zenye umuhimu zaidi, “tembea na simu ya smartphone iliyounganishwa na intaneti kwa bei yenye punguzo, ” alisema Wanyancha.

Bidhaa nyingine zitaonyeshwa na kampuni  siku ya nanenane, ambayo mwaka huu itafanyika kitaifa mkoani Lindi, bidhaa hizo ni pamoja na Tigo Kilimo – Huduma inayolenga  kukidhi mahitaji ya wakulima kwa kuwapa taarifa kuhusu upatikanaji wa mbolea, soko la mazao yao na utabiri wa hali ya hewa. 

Kampuni ya Tigo ndiyo mdhamini mkuu wa maonesho ya nanenane mwaka huu.

Tunawahimiza wakulima katika mikoa ya kusini ya Mtwara, Lindi na Pwani kutembelea banda letu na kujifunza juu ya jinsi ya kupata taarifa muhimu kwa urahisi kuhusu kilimo kupitia simu za mkononi,” alisema Wanyancha na kubainisha kuwa Tigo Kilimo pia inapatikana kupitia vipengele vya kwenye simu.

Mkutano wa waandishi wa habari ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa shirika la Tanzania Agricultural Society (TASO) Engelbert Moyo ambaye alisema kuwa, maonesho ya nanenane ya mwaka huu yatavutia washiriki kutoka sekta ya mawasiliano ya simu, madini, kusindika mazao, nishati, misitu, utalii, mifugo na sekta ya nyuki.

Taasisi zote muhimu za serikali pia zitashiriki maonesho ikiwa ni pamoja na wizara ya Kilimo chakula na Ushirika,Viwanda na Biashara, Maliasili na Utalii; Nishati na Madini, Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,Mambo ya Ndani, ulinzi, miongoni mwa wengine kama kawaida.

"Tunatarajia viongozi wakubwa wa serikali kutembelea maonesho ikiwa ni pamoja na Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein ambaye ndiye amepangwa kufungua rasmi maonesho ya nanenane mwaka huu," alisema Moyo.

No comments:

Post a Comment