KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 27, 2015

DKT. JOHN POMBE MAGUFULI:NINASIMAMIA NINACHOKIAMINI, NATAKA TANZANIA YENYE MABADILIKO BORA SIYO BORA MABADILIKO

????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli kiwahutubia wananchi wa mji mdogo wa Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya jana katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Tunduma na kuhudhuriwa maelfu ya wananchi, Dr. John Pombe Magufuli amewaomba wananchi wa Tunduma kura za ndiyo ili aweze kuongoza watanzania katika kupeleka gurudumu la maendeleo mbele zaidi.
Amesema ametumikia nchi hii kwa miaka 20 serikalini akiwa Waziri na amekuwa akisimamia kile anachokiamini kwamba ndiyo maendeleo ya watanzania, amekuwa mkweli, muaminifu kwa viongozi wake, mcha mungu na mchapa kazi hivyo anaomba nafasi ya urais ili aweze kuona Tanzania yenye mabadiliko bora kwa watanzania na siyo bora mabadiliko.
Uchaguzi mkuu wa jamhuri ya Muungao ya Tanzania wa Rais , Wabunge na Madiwani  unatarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu nchini kote, ambapo vyama mbalimbali vya siasa vinatarajiwa kushiriki katika uchaguzi huo(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-TUNDUMA)
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa mji mdogo wa Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya jana.
????????????????????????????????????
Uwanja wa shule ya msingi Tunduma ukiwa umefurika wananchi waliokuja kumsikiliza mgombea urais kupitia CCM Dkt. John Pombe Magufuli.             

No comments:

Post a Comment