Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA), imetoa onyo kali kwa Shirika la
Utangazaji (TBC1) kwa kuchambua vichwa vya habari vya magazeti kwa
upendeleo.
Kadhalika Redio ya Magic FM imepewa onyo kali huku ikitakiwa kulipa
faini ya Sh milioni 2.5 baada ya kukiuka maadili ya utangazaji kupitia
kipindi chake cha 'Morning Magic'.
Uamuzi huo ulitolewa jana jijini Dar es Salaam katika mkutano wa
waandishi wa habari wakiwemo wawakilishi kutoka TBC1 na Magic FM,
Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Wolter Byoga, alisema TBC1 kupitia
kipindi chake cha Jambo Tanzania, katika kipengele cha uchambuzi wa
magazeti kilikuwa kikiruka habari kubwa na kusoma ndogo.
No comments:
Post a Comment