Mwenyekiti mwenza wa UKAWA
James Mbatia (Pichani) amezungumza mchana huu na Waandishi wa
habari na kujibu baadhi ya mambo aliyosema Dkt.Wilbroad Slaa Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Slaa, Dkt Slaa katika hotuba yake aliuponda uamuzi wa Chadema wa kumsimamisha Waziri Mkuu wa zamani Mhe.Edward Lowassa, alisema Lowassa si mfasi na hafai kuwa Rais wa Tanzania.
Mbatia alisema "Napenda kuwaomba
Watanzania tusimame wote kupata Katiba mpya ambayo ndiyo ajenda ya mgombea wetu
Lowassa".
Mbatia aliwaomba Watanzania waelewe UKAWA tunasimamia utu, uzalendo, uadilifu, umoja, uwazi, uwajibikaji
ndani ya Tanzania.
Alisema Wanasiasa hasa wale
wa CCM Mwakyembe na Sita, wanaotaka midahalo waje waongee na mimi wasimsumbue
Mgombea wetu Lowassa sio saizi yao.
"Hivi ni viashiria
kwamba CCM wameshindwa hoja, mara kuleta mambo ya udini, mara wanaibua hili
mara lile. wanataka kuchafua amani yetu kwa kuigiza masuala ya dini," alisema
Alisema "Tukisema tuibue
masuala yote na kashifa za kuuzwa kwa nyumba, kuna mtu atabaki salama?
Dondoo za Mbatia wakati akizungumza na vyombo vya habari lei
Mbatia: Eti Lowassa akija
ndani ya Ukawa atakuja na Wenyeviti wa CCM..hakuwahi kusema..kayasemea wapi?
Mbatia: Wewe unasema ni
muadilifu ulipewa Milioni 500 mwaka 2008 unakuja kusema leo baada ya miaka 7?
Tuwe wakweli.
Mbatia: Eti suala la rushwa
zaidi ya miaka 7 usiripoti halafu uje useme leo, kusema uongo ni kazi sana.
Mbatia: Napenda kuwaomba
watanzania wote ambao ni zaidi ya milioni 46, wasiruhusu nchi yetu ikaharibiwa
na watu 100.
Mbatia: Wakenya walisema
hata kama ana makosa, walisema huyo huyo tunamtaka, wakampigia kura na leo ni
Rais wao.
Mbatia: Watu wachache
wanaotaka eti kwa lolote lile lazima waendelee kubaki madarakani, tunasema
hapana.
Mbatia: Lazima tufute mfumo
huu uondoke tuwe na Tanzania mpya.
Mbatia: Napenda kuwaomba
wale Viongozi wa dini walionewa kwa yale ya jana, wasamehe na waachane nayo.
Mbatia: Lowassa hajawahi
kutamka kuwa nikija ndani ya UKAWA nitakuja na wabunge 50, wenyeviti wa CCM na
Makatibu nk.
Mbatia: Kama hana faida
haya mafuriko tungepata wapi? Nyota ya Lowassa inang'aa hata wafanye nini
hawamuwezi huyu jamaa
Mbatia: Hatuna haja ya
kuanza kumjadili, hiyo ni kulipasua Taifa la Tanzania kwa maslahi binafsi
Mbatia: Kilichotusikitisha
ni yeye kuhusisha watu wengine wasiohusika kwenye jamii yetu, viongozi wa dini
wenye heshima zao, acha sisi vyama vya siasa tusuguane wenyewe.
Mbatia: Zimebaki siku 50 na
kitu, haki itendeki na nchi yetu ibaki na amani siku zote
Mbatia: Anasema kaja
kupambana na Lowassa kwakuwa anagombea urais, sasa Sumaye naye anagombea urais?
Mbatia: Nimesoma barua ya
ufisadi, ufisadi ni mfumo na Lowassa ana haki ya kujielezea lakini hawa wanataka kututoa kwenye reli tuanze kujibizana mmoja na wengine.
No comments:
Post a Comment