Mmiliki na Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya Black Sensation, Lilliane Masuka (katikati),
akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo
asubuhi, kuhusu Tamasha la Fahari ya Mwafrika litakalofanyika viwanja
vya Club ya Escape One, Oktoba 3, 2015 Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa kampuni hiyo, Gabriel Manyaga na
Mkurugenzi wa Ubunifu wa kampuni hiyo, Charlotte Mwaigwisya.
Mkurugenzi
wa Uendeshaji wa Kampuni ya Black Sensation, Gabriel Manyaga (kushoto),
akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Mmiliki na Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni hiyo, Lilliane Masuka.
Mkurugenzi wa Ubunifu wa kampuni hiyo, Charlotte Mwaigwisya akitoa ufafanuzi kwa waaandishi wa habari kuhusu tamasha hilo.


No comments:
Post a Comment