![]()  | 
Mwenyekiti
 wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, amesema kwa sasa kila chama kipo 
kwenye kampeni za kutafuta ushindi, hivyo kauli kama hiyo inaweza 
kutolewa na upande wowote ikiwa ni mbinu ya kujipatia ushindi.
“Ingekuwa
 kauli yake tafsiri yake ni kuwa hawatakubali matokeo ya uchaguzi hapo 
tume ingekuwa imehusika na ingezungumza kwa kuwa tulishasema kila chama 
shindani katika uchaguzi huu kinatakiwa kukubali matokeo 
yatakayotangazwa na tume,” alisema.
Alisema hadi sasa NEC haijaona cha kujibu juu ya kauli hiyo na inaichukulia ni matamshi ya kisiasa ya kampeni.
Hivi
 Karibuni Bulembo akiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika mjini 
Kigoma, alidaiwa kutoa kauli kuwa chama chake hakitakuwa tayari kuiachia
 Ikulu kwa namna yoyote ile.
Mwenyekiti
 wa Ukawa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, 
akizungumza na waandishi wa habari, juzi alilalamikia kauli hiyo na 
kuitaka NEC kulaani kauli hiyo kwa kuwa uchaguzi ni ushindani na hakuna 
mwenye maamuzi zaidi ya wapiga kura.



No comments:
Post a Comment