KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 22, 2015

WADAU WA MICHEZO WATAKIWA KUISAIDIA SERIKALI KUKUZA MICHEZO KUFUFUA VIPAJI VYA WACHEZAJI

unnamedH
KAIMU Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mushi (Kulia) akikadhi cheti cha Tuzo kwa mdau, Abbas Ally wa Kampuni ya Isere Sports inayouza vifaa vya michezo aliyeshiriki kufanikisha mkoa wa Dar es Salaam kutwaa ubingwa wa jumla katika mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) ysaliyofanyika mkoa wa Mwanza mapema mwaka huu na DAr es Salaam kutwa ushindi wa jumla kwa kujikusayia medali 26.

……………………………..
Na Mwandishi Wetu

WADAU wa Michezo mkoa wa Dar es Salaam wametakiwa kujitokeza kuisaidia Serikali kukuza michezo na kufufua vipaji vya wachezaji katika fani mbalimbali katika shule za msingi na Sekondari.

Akizungumza katika sherehe ya kuwapongeza wachezaji na wadau mbalimbali walioshiriki michezo ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) Dar es Salaam juzi,Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mushi aliwataka wadau wa michezo kujitokeza kusaidia Serikali kufufua vipaji vya wachezaji kutoka ngazi ya shule ya msingi na sekondari.

Mushi alimpongeza Rais Jakaya Kikwete anayemaliza muda wake kurudisha michezo hiyo mashuleni baada ya kuondolewa katika uongozi wa RAis Mpaka hivyo kuathiri vipaji vya vijana wengi kushindwa kung’ara katika medani ya michezo nchini.

Katika sherehe hizo ambazo mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam waliokuwa ukipongezwa kwa kutwaa ubingwa wa jumla za mashindano hayo yaliyofanyika mkoa wa Mwanza mapema mwaka huu,Meneja wa timu ya UMITASHUMTA ya Mkoa wa Dar es Salaam, Adolf Ally alisema haikuwa rahisi kupata ushindi huo kwa sababu mikoa mingi ilidhamiria kupata ushindi huo lakini wao walijiandaa zaidi kwa kushirikiana na wadau.

Mkurugenzi wa MAsoko wa Kampuni ya Isere Sports, Abbas Ally ambao ni wauzaji wa vifaa michezo nchini aliyepata tuzo ya wadau waliofanikisha kupatikana kwa ushindi huo aliahidi kuongeza vifaa vyenye ubora kwa bei nafuu ili mwakani mkoa huo uendelee kuwa mabingwa.

Aliwaomba wadau wengine kujitokeza kusaidia michezo ili kurejesha hadhi ya michezo katika shule za msingi na Sekondari ili kujenga timu imara za Ligi Kuu na timu ya Taifa ya Tanmzania (Taifa Stars).

Mkoa wa Dar es Salaam uliochukua ushindi wa jumla kwa kutwaa medali  26 katika michezo mbalimbali lakini ikiwemo soka ya wanawake lakini ilijikuta inafungwa katika mchezo wa soka ya wamaume baada ya kupachikwa bao 1-0 na wenyeji Mwanza.

No comments:

Post a Comment